Mwanajeshi mstaafu Marekani, anawania ubunge Marakwet Magharibi-Benson Cheserek
Siasa na Gumzo
Jan. 18, 2022
Benson Cheserek ni miongoni mwa Wakenya ambao wanaishi ughaibuni (Kenyans in diaspora) na sasa analenga kuwania kiti cha ubunge kwenye eneo la Marakwet Magharibi katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet. Cheserek amekuwa akiishi Marekani kwa miaka 17 ambapo amefanya kazi katika jeshi la Marekani kwa miaka 8 kabla ya kuanza biashara yake binafsi. Kwenye mahojiano na mwanahabari Faith Kutere, Cheserek anasema analenga kutumia ujuzi wake katika idara ya usalama kusaidia kukabili ukosefu wa usalama kwenye Bonde la Kerio, kubadili maisha ya wakazi wa eneo la Marakwet Magharibi kupitia masomo miongoni mwa masuala mengine.
RELATED EPISODES
Kujiunga kwa ODM Na Serikali Kutakomesha Maandamano ya Gen Zs?
Hasla Akosa Usingizi Kufuatia Gharama ya Maisha | Siasa na Gumzo Podcast
Uteuzi wa Makatibu Wazua Tumbojoto, Raila akitaka Waluke Kuachiliwa | Siasa na Gumzo Podcast