Elimu Podcast: CBC Yawapa Taabu Wazazi, Walimu na Wanafunzi
Elimu
Sep. 07, 2021
Malalamishi kuhusu Mtalaa wa Umilisi, CBC yanazidi kuongezeka. Wazazi wanalalamikia gharama ya juu ya vifaa vya masomo vilevile kulalamikia suala la kutumia muda mwingi kuwasaidia wanao kufanya mazoezi waliyopewa shuleni. Baadhi yao wanapendekeza kusitishwa kwa mtalaa huo na kurejelewa kwa ule wa 8.4.4. Walimu nao wanalalama kwamba hawakupewa mafunzo yafaayo kuhusu CBC mbali na kuhitajika kufanya kazi za ziada. Wanafunzi pia wanalazimika kubeba vitabu vingi mno na kuhangaika kutafuta vifaa vinavyohitajika shuleni. Shadrack Miti amezungumza na pande zote zinazohusika. Sikiliza podcast hii kwa kina chake.
RELATED EPISODES
CBC irekebishwe; Humphrey Obarah
Wanafunzi pacha; alama sawa, KCPE na KCSE
Elimu ya kiufundi Ukraine; fursa za ajira ni chache - Paul Kurgat
Elimu: Siku ya Kiswahili Duniani (UNESCO); tukitumie ofisini, siasani....