Hoja za Wahariri Podcast: Raila ni chaguo la Uhuru, huku siasa zikichacha Mlima Kenya
Hoja za Wahariri
Aug. 13, 2021
Rais Uhuru Kenyatta amewasihi wanasiasa wa One Kenya Alliance kumuunga mkono Raila Odinga kuelekea uchaguzi mkuu wa 2022, huku pendekezo lake likikataliwa vikali na wanasiasa hao. Aidha, wanasiasa mbalimbali wanazidi kujitokeza kwenye eneo la Mlima Kenya wakishindania udhibiti wa siasa za eneo hilo, Uhuru anapoelekea kustaafu. Je, kati ya William Ruto na Raila Odinga, ni nani atakayenufaika katika siasa za Mlima Kenya na ni nani atakayepoteza? Eneo la Mlima Kenya litaamua siasa za 2022? Wawaniaji wa urais wawateue wagombea wenza kutoka maeneo gani ya nchi? Mhariri, Geoffrey Mung'ou na wanahabari wa Standard - Chris Thairu na Mike Nyagwoka wanayapambanua masuala haya.
RELATED EPISODES
Vita vya Urusi na Ukraine; athari kwa dunia
Mzozo wa Urusi na Ukraine; Mohamed Abdul-Rahman anachambua
Hoja za Wahariri: Kitendawili cha mili Mto Yala - ndani ya magunia